Wednesday 16 May 2018

MALANGO/MILANGO

BWANA YESU ASIFIWE

Napenda nikutakie mafanikio makubwa sana kwenye maisha yako mtu wa Mungu.
Lakini ndani ya wewe kupata mafanikio inabidi uzijue baadhi ya Siri ambazo Roho atazifunua kwetu leo.

Inabidi kwanza ujue kwamba kila mafanikio ambayo yanakuja kwako kuna mlango ambao huwa yanapitia ili kukufikia na ni kusudi la Mungu wewe ufanikiwe.

3YOHANA 1:1-2
Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli.
Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.

***************

Hizi ni baraka ambazo Yohana alikuwa akimbariki mzee Gayo ambae inaonekana alikuwa amefanikiwa kwenye mambo ya kiroho lakini kimwili bado.
Hivyo Yohana akawa anamtamkia baraka zidhihirike katika ulimwengu wa mwili.

KWANINI ALIKUWA HAJAFANIKIWA KIMWILI?
Ule mlango ambao baraka na mafanikio yake ilitakiwa yapitie inaonekana adui alikuwa amesimama kuhakikisha anazuia mafanikio yake kimwili kama vile, afya, elimu, maendeleo n.k
Napozungumza kuhusu mafanikio ni zaidi ya pesa, majumba na magari.

Maana unaweza ukaona watu wanamiliki hivyo vyote lakini bado ni mgonjwa wa maradhi yasiyotibika.
Mafanikio anayotakiwa kufanikiwa mtu yaliyo kusudi la Mungu ni kumiliki vyote na kuwa na uzima wa kiroho yaani maelewano mazuri wewe na Mungu.

MALANGO

MALANGO yako yanapomilikiwa na adui huwa anapitisha mambo yake kama magonjwa, umasikini na mengine yote yanayotesa maisha ya binadamu.
Pia yanapofungwa hutaweza kupata chochote maana yatakuwa hayapitishi chochote.
Chochote kile kinachokutokea ukakiona kwa macho yako ni lazima kiwe kimepitia kwenye hayo MALANGO katika ulimwengu wa Roho ndipo yadhihirike katika ulimwengu wa Mwili.

MATHAYO 16:18-19
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lolote utakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.

********************

Hayo ni maneno Yesu alikua akimwaambia Petro.
Kwamba kanisa atakalosimamisha yeye halitashindwa na MILANGO ya kuzimu.
Kanisa ni mimi na wewe rafiki. Yesu anasema hatutashindwa na vita ya kuzimu maana ametupa sisi funguo za kufungua hiyo MILANGO iwe wazi na baraka zipate kuingia.

MILANGO au MALANGO yako ikishamilikiwa na adui kamwe hutaweza kuona baraka zozote katika maisha yako.

MWANZO 22:17
Katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani, na uzao wako utamiliki MLANGO wa adui zao.

****************

ZABURI 115:10
Enyi mlango wa Haruni, mtumainini BWANA; Yeye ni msaada wao na ngao yao.

********************

ZABURI 24:9
Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Naam, viinueni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.

***************

Kwa hivyo vifungu hapo juu nadhani utakuwa umeshapata picha juu ya uhusiano wa malango na upitishwaji wa baraka zako.

MALANGO au MILANGO yako inatakiwa iwe wazi na pia anaetakiwa kuwa hapo kama msimamizi ni mfalme wa utukufu ili apitishe mambo mema katika maisha yako.
Tumeona kabisa Mungu alivyomwaambia Ibrahimu kwamba mlango wake utamiliki mlango wa adui.

Pia Haruni anaambiwa mlango wake umtumaini BWANA.

ISAYA 60:11
Malango yako nayo yatakuwa wazi daima;
Hayatafungwa mchana wala usiku;
Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa,
Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

******************

MILANGO yako inatakiwa iwe wazi na imtumainie Mungu.

Na pia tumeona hapa kuwa agano la kumiliki milango Mungu analifanya na Ibrahimu

Kwanini amefanya hilo agano na Ibrahimu?

Mungu amefanya agano na Ibrahimu kwamaana yeye ni mwaanzilishi wa taifa la Israeli.
Kwahiyo rafiki yangu katika maisha yetu sisi ni uzao wa Ibrahimu kiroho.
Tunatakiwa kabisa kuzirithi baraka za Ibrahimu.

Tunaona Ibrahimu anafanikiwa.

Isaka anafanikiwa.

Yakobo anafanikiwa.

Huo ni ukoo wa Ibrahimu ambao mwanzilishi wa huo ukoo ambae ni yeye huyo Ibrahimu MALANGO yake yalimtumaini Mungu.

WEWE MWAANZILISHI WA UKOO WENU ALISIMAMISHA NINI KWENYE MILANGO YENU?
 ALIMTUMAINI NANI?

Haruni aliinua kichwa ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
Je, kwenye ukoo wenu mwaanzilishi aliinua vichwa ili nani apite?

ALICHINJA MBUZI?

ALIOMBA MIZIMU?

ALITAMKA MANENO GANI?

Hilo ni swali la kujiuliza.

Omba Roho mtakatifu akufunulie maana yeye huchunguza yote hata mafumbo ya Mungu.

TUNATOKAJE?
Yesu alishasema hatakubali kanisa lake lishindwe na milango ya kuzimu,
Na kanisa la Kristo ni mimi na wewe tuliyempokea.
Hatutashindwa juu ya hiyo milango ya adui ya huko kuzimu ya kupitisha uharibifu kwa watu wake.
Tuna funguo za kufunga na kufungua ambazo ni yeye mwenyewe.

YESU NDIYE FUNGUO.
Kama umempokea na yeye akakaa ndani yako atafunga na kufungua na atafungua milango yako na kufunga ile ya kuzimu.

Haya yote ni mambo ya rohoni na hayaonekani kwa macho ya nyama.
Kuzimu ni ufalme ambao anaishi shetani na milango ya shetani ipo na inapitisha laana na uharibifu wake wote.
Lakini pia upo ufalme wa Mbinguni ambao ni wa Yesu Kristo na mlango wa huko mbinguni ni Yesu Kristo pekee.

Hivyo hizo falme mbili huwa zinafanya kazi kwetu sisi.
Ufalme wa mbinguni ukitubariki na kuzimu ukitulaani.

Tunamshukuru Mungu baba kwa jina la Yesu Kristo kwani ametupa mamlaka ya kuharibu na kuvunja ngome zote huko kuzimu.

WAEFESO  6:11-17
Vaeni silaha zote za Mungu, Mpate kuweza kuzipinga hila za shetani.
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; Bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu.

*******************

WOKOVU TUNAO, SILAHA TUNAZO, FUNGUO TUNAZO NA MAMLAKA PIA TUNAYO

Tunasubiri tena nini watu wa Mungu?

NAWATAMKIA BARAKA ZOTE KWA JINA LA YESU KRISTO.

AMEN.

POWERED BY HOLLY SPIRIT

Saturday 12 May 2018

OMBA HALAFU CHUKUA HATUA USISUBIRI MUUJIZA.

BWANA YESU ASIFIWE SANA

ASANTE SANA ROHO MTAKATIFU KWA KUNIFUNULIA MIMI MTOTO MCHANGA NA KUWAFICHA WENYE HEKIMA NA AKILI ZAO.

1WAKORINTHO 1:18-19
Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.

 Kwa kuwa imeandikwa,Nitaiharibu hekima yao wenye hekima,Na akili zao wenye akili nitazikataa.
"
"
"
LEO ROHO MTAKATIFU ANATUFUNDISHA NENO LENYE KICHWA KINACHOSEMA.

OMBA HALAFU CHUKUA HATUA USISUBIRI MUUJIZA.

Hili nambo la kuchukua hatua limekuwa ni changamoto kubwa sana kwa watu wanaomwamini Mungu.

Uwezo wa kufanya chochote tena katika mazingira yoyote upo kwa Mungu wetu wa mbinguni lakini Mungu anapenda sana uchukue hatua.

Ndiyo maana hata yeye katika kutuletea WOKOVU anasema

YOHANA 3:16
Kwa maana jinsi hii Mungu alivyoupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, Bali awe na uzima wa milele.
"
"
"
Mungu angeweza kusema tu kwa maneno kwamba

 "NIMESHAWAPA WOKOVU"

Lakini alichukua hatua na ikaonekano mbele za macho ya watu.

TWENDE KWENYE MSINGI WA MAFUNDISHO YETU YA LEO.

YAKOBO 2:17
Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake.
"
"
"
Usikae tu ukimuomba Mungu kwa imani bila kuchukua hatua ya kuufuata muujiza unaoutafuta.
Wana wa Israel wasingeweza kusimama pale Misri kwa imani halafu wakajikuta wapo nchi ambayo Mungu aliwaapia baba zao kwamba itakuwa yao.

Usije ukakaa ukimuomba Mungu akupe kazi ya kulipwa mshahara mkubwa na wakati huna hata juhudi za kuitafuta yenye mshahara mdogo.

Usije ukamuomba Mungu kwa imani yako akupe Mume/Mke mwema na wakati wewe ni waruwaru.
Yani unataka mtu mkarimu na mstaarabu na wakati wewe ni mchoyo na hujatulia.
Kumbuka Mungu alisema atakupa wa kufanana na wewe.

CHUKUA HATUA
Wana wa Israeli bila kuchukua hatua wasingeirithi ile nchi.
Wana wa Israeli mpaka kuifikia ile nchi ya ahadi walikutana na vikwazo vingi sana njiani.
Mungu alikuwa anaviona lakini aliviacha ili watakapochukua hatua ya kupambana navyo nae aingilie kati kuwasaidia.

YOSHUA 24:7-8
Nao walipomlilia BWANA, akaweka giza kati ya ninyi na Wamisri, akaileta bahari juu yao, akawafunikiza; nayo macho yenu yaliyaona mambo niliyoyatenda huko Misri; kisha mkakaa jangwani siku nyingi.

 Kisha nikawaleta na kuwaingiza katika nchi ya Waamori waliokaa ng’ambo ya pili ya Yordani; nao wakapigana nanyi; nikawatia mikononi mwenu, mkaimiliki nchi yao; nami nikawaangamiza mbele yenu.
"
"
"
Jambo lolote unalotaka Mungu akutendee pamoja na kuomba inatakiwa uchukue hatua.
Sasa wewe kaa nyumbani halafu umuombe Mungu kwamba unatafuta kazi utaona matokeo yake.

Wewe kijana endelea kupanga wanawake foleni ukifikiri ni sifa au kuna tunzo utapata halafu umuombe Mungu akupe mke mwaminifu ukifikiri kuna muujiza utatokea.

Na wewe msichana endelea kuvaa nguo zisizo na maadili kabisa na kubadilisha wanaume kila siku huku ukimuomba Mungu mwanaume mwenye akili zake timamu ufikiri kuna muujiza utatokea.
Ukikaa mahali popote unaongelea ngono tu na maneno machafu yanatoka kwenye kinywa hichohicho unachokitumia kumuitia Mungu kwenye matatizo yako.
"UTAMPATA WA KUFANANA NA WEWE"

Kila jambo unaloliombea lazima uchukue hatua ndipo Mungu nae ataingilia kati.

KUTOKA 14:13-14
Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

 BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
"
"
"
Tazama hapo Musa amewajengea imani ambayo Mungu hakukubaliana nayo.
Alivyowaambia "simameni tu"
Kumbe japo Musa alikuwa na imani sana na Mungu kwamba lazima atawaokoa lakini hakupaswa kuwaambia wasimame.
Angalia Mungu alichomwambia Musa baada ya kuwaambia wana wa Israeli "simameni tu"

KUTOKA 14:15-17
BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele.

 Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya; nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu.

 Nami, tazama, nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao wataingia na kuwafuatia, nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote, kwa magari yake na kwa wapanda farasi wake.
"
"
"
Kwa imani Musa aliwaambia "simameni tu"
Lakini Mungu akamwambia Musa "mbona unanililia mimi? "Akiwa na maana kwamba hakutakiwa asimamishe wale watu.
"Waambie wana wa Israeli waendelee mbele"
Mungu hataki mtu asimame, aache kuchukua hatua kwenye jambo lolote awe anamlilia yeye.
Mungu anasema kabisa atajipatia utukufu kwa farao pindi wana wa Israeli watakapopita kwenye njia kati ya bahari.
Ataifanya mioyo ya wamisri kuwa migumu.
Na hapo walipowafuata ndiko kulikokuwa kuangamia kwao na kweli Mungu akajipatia utukufu.

Hata wewe unapomuomba Mungu jambo lolote kwa imani ni lazima uchukue hatua mtu wa Mungu.

CHUKUA HATUA UTAONA MUNGU ANAVYOFANYA KAZI KUBWA SANA KATIKA MAISHA YAKO.

Kuna mambo ambayo huwa unamwomba Mungu wewe unafikiri bado hajakujibu ila ni kwa vile hujafuatilia ndipo akuonekanie katika jitihada zako.

HESABU 13:32-33
Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.

 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.
"
"
"
Wale walioenda kuipeleleza ile nchi waliwaletea habari mbaya ambazo ni za kishetani ili wasiende.

Kuna namna unataka kujaribu lakini unajiona wewe si chochote katika hilo jambo unalotaka kulifanya.
Unaanza kujiona dhaifu unaogopa.

Waliwaletea habari za ile nchi kwamba walipowaona hao Wanefili wana wa Anaki waliotoka kwa hao wanefili walianza kujiona nafsi zao kama mapanzi nao wakawaona hivyo hivyo.

METHALI 23:7
Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
"
"
"
METHALI 18:21
Mauti na uzima huwa katika uweza wa ulimi, na wao waupendao watakula matunda yake.
"
"
"
Jinsi unavyojishusha na kuogopa kuchukua hatua ya kufuatilia kile unachomuomba Mungu ujue ndivyo unavyoshushwa pia.

HESABU 14:9
Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope.
"
"
"
Ona sasa kumbe kile wanachokiogopa wao ni chakula chao.
Usitishike na majira na nyakati ngumu katika maisha yako.
Usiangalie watu wanasema nini ili kukuvunja moyo katika jitihada zako.
Haya mambo yalikuwepo tangu zamani.
Yupo Mungu mbinguni anayetutia nguvu wewe chukua hatua, amka uifuate ndoto uliyoiota.

KUTOKA 23:27
Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.
"
"
"
Kwanza unapomwendea Mungu usiangalie ukubwa wa tatizo ulilonalo,
Bali angalia na kutafakari ukubwa wa Mungu unaemwamini katika hiyo changamoto yako.
Muombe Mungu kwa imani kwamba unataka akupe kazi kwenye ofisi fulani halafu chukua hatua nenda pale kaombe kazi.
Usiwaogope hao Wanefili wana wa Anaki waliotoka kwa hao Wanefili.
Utawakuta hapo lakini ujue hao ni chakula kwako.
Usijione kama panzi mbele yao maana nao watakuona hivyo hivyo.

Mungu ameshawafadhaisha na kuvifadhaisha vyote katika kumuomba kwako lakini tatizo lipo kwako hujachukua hatua ukawafikia na utisho tayari upo mbele yao.
Chukua kibali chako nenda kwa kujiamini ukiwa na matumaini na Mungu wako halafu utauona wokovu wake BWANA wa Majeshi akijipatia utukufu wake.

Usiogope ukubwa wa ofisi

Usiogope ukubwa wa meneja mwajiri

Usiogope suti zao

YAMKINI CHANGAMOTO YAKO NI UGONJWA

Usiogope ukubwa wa ugonjwa

Usiogope majibu ya daktari maana hayazidi majibu yatokayo kwenye kiti cha enzi kwa Mungu wetu.

Jina la Yesu linazidi jina la ukimwi

Jina la Yesu linazidi jina la kansa

WAFILIPI 2:9
Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
"
"
"
Kwa jina la Yesu hakuna jina liwalo lote linaloweza kusimama na kushindana nalo.
Jina la Yesu linazidi majina yote.

Ni shetani anakupa utisho tu na kukuambia hii ofisi kubwa hivi usiingie wala hutapata msaada.

Huu ugonjwa mkubwa hivi wala usihangaike kutafuta uponyaji maana hutapona

Au vitu kama hivi siyo saizi yako waachie watu fulani maana utavihangaikia bure wala hutafanikiwa unapoteza muda wako.

METHALI 3:4-5
Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,
Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,
Wala usizitegemee akili zako mwenyewe.
"
"
"
Unatakiwa umtumaini BWANA kwa moyo wako wote na uwe na imani kwamba anaweza Jambo lolote.
Pia utumie akili maana yeye anasema

ISAYA 48:17
Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.
"
"
"
Kwanini Mungu anasema anakufundisha ili upate faida?  Inamaana utazitumia hizo akili na maarifa anayokupa.
Akili nzuri anayokupa Mungu inabidi uitumie.
Mbele zake na mbele ya mwanadamu ili ufaidike.

Unapaswa kutumia sana akili zako pamoja na kumtumaini Mungu.
Lakini hupaswi kuzitegemea kabisa hizo akili maana anasema pia amezikataa akili zao wenye akili na hekima yao wenye hekima ameiharibu.

"TUMIA AKILI NA MAARIFA YAKO YOTE LAKINI USITEGEMEE VITU HIVYO MTEGEMEE MUNGU."

Kila mtu aliyemtumaini Mungu alishinda baada ya kuchukua hatua.

ESTA 4:15-17
Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai,

 Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.

 Basi Mordekai akaenda zake, akafanya yote kama vile Esta alivyomwagiza.
"
"
"
Esta anawaambia watu wafunge na kuomba ili Mungu awaokoe wayahudi na hukumu iliyokuwa mbele yao.
Lakini pia Esta anasema atachukua hatua ataingia kwa mfalme kinyume cha sheria.
Siyo kwamba aliomba tu kwa imani na kusubiri ule waraka wa Hamani ubatilishwe kimuujiza.
Namna ambayo Esta alitaka kuingia kwa mfalme siyo rahisi kama unavyofikiria ndiyo maana Esta anasema kinyume cha sheria na akiangamia na aangamie.
Lakini ilibidi achukue hatua ili BWANA ampiganie.

ESTA 5:2-3
Ikawa, mfalme alipomwona malkia Esta amesimama uani, yeye akapata kibali machoni pake; naye mfalme akamnyoshea Esta fimbo ya dhahabu aliyokuwa nayo mkononi. Basi Esta akakaribia, akaigusa ncha ya fimbo.

 Mfalme akamwambia, Malkia Esta, wataka nini? Nayo ni haja gani uliyo nayo? Utapewa hata nusu ya ufalme.
"
"
"
Tazama baada ya Esta kuingia uani kwa mfalme ndipo mfalme alimwona akapata kibali machoni pake.
Kitendo cha kumwona tu Esta akapata kibali machoni pake.
Je, asingemwona angepata kibali?

ESTA 7:1-10
Basi mfalme na Hamani walikuja kula karamu pamoja na malkia Esta.

 Mfalme akamwambia Esta tena siku ya pili pale pale penye karamu ya divai, Malkia Esta, dua yako ni nini? Nawe utapewa; na haja yako ni nini? Hata nusu ya ufalme utafanyiziwa.

 Ndipo malkia Esta alipojibu, akasema, Mfalme, ikiwa nimepata kibali machoni pako, na mfalme akiona vema, nipewe maisha yangu kuwa dua yangu, na watu wangu kuwa haja yangu.

Maana tumeuzwa, mimi na watu wangu, ili tuharibiwe, na kuuawa, na kuangamia. Kama tungaliuzwa kuwa watumwa na wajakazi, ningalinyamaza; ila hata hivyo msiba wetu haulinganishwi na hasara ya mfalme.

 Ndipo mfalme Ahasuero aliponena, akamwambia malkia Esta, Ni nani huyu, tena yuko wapi, ambaye moyoni mwake alithubutu kufanya hivi?

 Esta akasema, Ni mtesi, tena ni adui, ndiye huyu Hamani, mtu mbaya kabisa. Mara Hamani akaingiwa na hofu mbele ya mfalme na malkia.

Mfalme akaondoka katika ghadhabu yake kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.

 Kisha mfalme akarudi kutoka katika bustani ya ngome hata mahali pa karamu ya divai. Ikawa Hamani amejitupa chini penye kitanda alipokuwapo Esta. Mfalme akasema, Namna gani! Je! Atamfanyia malkia jeuri hata machoni pangu nyumbani mwangu? Na neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, wakamfunika uso Hamani.

Ndipo aliposema Harbona, msimamizi-wa-nyumba mmojawapo wa wale waliohudhuria mbele ya mfalme, Tazama, basi, mti wa mikono hamsini urefu wake, Hamani aliomwekea tayari Mordekai, ambaye alinena vema kwa ajili ya mfalme, upo umesimamishwa nyumbani kwa Hamani. Mfalme akasema, Mtundikeni juu yake.

 Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.
"
"
"Maombi ya Esta na wayahudi Mungu aliyasikia sana.
Hatua za Esta zilimbadilishia kifo cha Mordekai.
Hamani akaangamia kwenye mti aliomwandalia Mordekai kutundikiwa.

Ukikaa vizuri na Mungu na ukilijua neno lake linasema nini huwezi kuangamia kwa jina la Yesu.
Wewe unaamua mwenyewe je,
Hao wachawi unataka uangamize uchawi wao?  Au unataka walichotuma kwako uwarudishie waangamie wenyewe?
Au unataka uzuie kabisa na kupiga marufuku nguvu zozote za kichawi kukufuatilia?

Kila unachotaka kukifanya hapa duniani majibu yapo kwenye BIBLIA yako.

NAKUTAKIA MWANZO MPYA NA USHINDI WA KISHINDO KATIKA JINA LA YESU KRISTO.
USIANGAMIE KATIKA MITEGO YAO.
MASHIMO WALIYOKUCHIMBIA WAKADUMBUKIE WAO WENYEWE.
ANZA SASA KUCHUKUA HATUA HUKU UKIMTUMAINI YEYE NA HAUTA AIBIKA MILELE.
NIMEOMBA NIKIAMINI NA KUSHUKURU KATIKA JINA LA YESU KRISTO.
AMINA.

#Powered_by_Holly_Spirit

Thursday 10 May 2018

MUNGU HUBARIKI KULINGANA NA MAPENZI YAKE NA NJIA ZAKE SI NJIA ZETU. PIA AKILI ZAKE HAZICHUNGUZIKI.

BWANA YESU ASIFIWE SANA.

Leo nakuletea somo lenye kichwa kinachosema,

MUNGU HUBARIKI KULINGANA NA MAPENZI YAKE NA NJIA ZAKE SI NJIA ZETU.
PIA AKILI ZAKE HAZICHUNGUZIKI.

Lengo la Mungu kumuumba mwanadamu pamoja na vyote alivyopendezwa navyo kwamba viwepo ni ili vimwabudu tu.
Hukuumbwa kwaajili ya kufanya jambo lingine lolote pasipo kulitukuza jina lake.

WAKOLOSAI 3:17
Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

**** **** ****
Haijalishi unafanya mizaha,
Haijalishi unaongea na marafiki zako,
Haijalishi unajenga nyumba,
Wala haijalishi unafanya jambo gani.
Lazima ufanye kwa jina la Bwana Yesu.

Vyote mwanadamu anavyovihangaikia hapa duniani vinatakiwa viwe ni matokeo ya kumwabudu Mungu na siyo umwabudu ili akupe hivyo vitu.
Unaweza ukamtafuta sana Mungu kwa muda mrefu ukahisi bado hujabarikiwa lakini nakuambia Mungu anabariki jinsi apendavyo.
Unaweza ukawa umeshabarikiwa lakini kulingana na namna unavyojiona na watu wanavyokuona unahisi bado hujabarikiwa.
Unachotakiwa kushikilia kwenye akili yako ni kwamba,

Mungu akupe mali au la asikupe mali ni lazima umwabudu yeye.

Akupe hitaji lako, la asikupe ni lazima umwabudu yeye tu.

Akubariki la asikubariki ni lazima umwabudu yeye.

Mtume PAULO alikuwa na nguvu nyingi sana za Mungu ndani yake.
Lakini pamoja na hayo pia alikuwa na udhaifu ndani ya mwili wake.
Uthaifu aliokuwa nao PAULO ni udhaifu ambao aliweza kuuondoa katika mwili wa mtu mwingine kwa jina la YESU na huyo mtu akapokea uponyaji akapona.
Lakini kwake ilishindikana kuuondoa kwa jina la huyo huyo YESU.

2WAKORINTHO 12:7-10
Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.

 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.

 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

**** **** ****

Mungu akawa anajisifu na udhaifu wa PAULO kwamba uweza wake utatimilika ndani ya udhaifu huo huo.

Je, Paulo alikuwa hajabarikiwa na Mungu?

Unaweza ukawa karibu sana na Mungu lakini bado ukawa na mizigo ya changamoto usizoweza kuziepuka katika maisha yako.
Shetani atakubeza (Mungu wako yuko wapi katika hili unalopitia?)
Ili usijisifu tena na huyo Mungu.
Lakini mwambie shetani kwa ujasiri kwamba "MUNGU HUBARIKI KWA MAPENZI YAKE"
Hata sasa Mungu yupo na mimi na ninatembea katika baraka zake.
Na jinsi mwanadamu aonavyo sivyo Mungu aonavyo.
Ilimradi unaishi katika kusudi la Mungu kukuumba wewe la kumtumikia na kumwabudu yeye peke yake.
Ikiwa unaishi kwa misingi ya neno lake basi usijali changamoto na kejeli zozote za shetani wewe amini Mungu yuko na wewe na amekushika mkono.

TWENDE SASA KWENYE NENO LA MSINGI WA MAFUNDISHO YETU.

ISAYA 55:8
Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.

**** **** ****
Hilo ndilo neno letu la msingi wa MAFUNDISHO yetu. Tuangalie Roho Mtakatifu anatufundisha nini juu ya hili neno.

Unapomwabudu Mungu kwaajili ya shida fulani unakuwa kama unamtaka MUNGU ainunue haki yake kutoka kwako.
Utakuwa kama unataka kumhonga kitu ambacho ni haki yake.
MUNGU ni MUNGU tu na anapaswa kuabudiwa hata kama hajatatua changamoto zako isikiondoe wewe katika kusudi la yeye kukuumba.
Hata kama humtimizii mtoto wako mahitaji yake yote haitaubadilisha ukweli uliopo kwamba wewe ni baba yake.
Atakuamkia shikamoo baba,
Atakuheshimu na hataweza kubadili damu usiwe baba yake.

MUNGU HUBARIKI KWA MAPENZI YAKE JINSI APENDAVYO YEYE.
lakini zote ni baraka.

Mwenye maono amebarikiwa
Anaeponya kwa jina la YESU amebarikiwa
Mwenye Mali amebarikiwa na mwenye afya nzuri pia amebarikiwa.
Yupo mwenye treni, meli, ndege na migodi ya madini ambae amebarikiwa na Mungu ikiwa analiishi neno lake.
Lakini yupo pia mwenye mifugo, mashamba, familia imara na Hana elimu naye amebarikiwa.
Wote wamebarikiwa KULINGANA na MAPENZI ya MUNGU.

MATHAYO 4:10
Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

**** **** ****
Tunachokiangalia tu ili tujue tumebarikiwa ama hatujabarikiwa ni je,
Tunaishi katika misingi ya NENO la MUNGU?
Kama unapitia changamoto na vikwazo vingi na wakati huo unamwabudu Mungu wala usitishike na hizo changamoto.
Hata Yesu huyo mjaribu alimjia kwakuwa alikuwa kwenye wakati mgumu lakini yeye hakutoka katika kusudi la Mungu.
Alimshinda kwa NENO.

JIFUNZE SASA NAMNA AMBAVYO MAWAZO YA MUNGU YALIVYO TOFAUTI NA MAWAZO YETU.

YOSHUA 24:2-3
Yoshua akawaambia watu wote, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Baba zenu hapo zamani walikaa ng’ambo ya Mto, maana Tera, baba yake Ibrahimu, naye ni baba yake Nahori; wakaitumikia miungu mingine.

 Nami nikamtwaa Ibrahimu baba yenu toka ng’ambo ya Mto, nikamwongoza katika nchi yote ya Kanaani; nikaongeza uzao wake, nikampa Isaka.

**** **** ****
Mungu alimtoa Ibrahimu ndani ya nyumba ya baba yake Tera waliokuwa wanaabudu miungu.
Lengo la Mungu ni kumtengeneza Ibrahimu  aanzishe uzao mwingine ambao ungemtumikia na kumwabudu yeye.

Asilimia kubwa watu waliabudu miungu mingine na hilo jambo halikumpendeza Mungu aliye hai.

MWANZO 12:1-3
BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.

**** **** ****
Hizi ni baraka za ajabu sana ambazo alikuwa anazijuwa Abram peke yake pamoja na Mungu aliyemwahidi.
Na alikuwa anajijuwa kwamba amebarikiwa kwa kiwango kikubwa sana.
Lakini hakujuwa kuwa hizo baraka zitakuwa za aina gani.
Akayafuata maagizo ya Mungu akajitenga na nyumba ya baba yake Tiro waliokuwa waabudu miungu.
Akaenda kumwabudu Mungu aliye hai.

MWANZO 13:15-16
maana nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao wako hata milele.

 Na uzao wako nitaufanya uwe kama mavumbi ya nchi; hata mtu akiweza kuyahesabu mavumbi ya nchi, uzao wako nao utahesabika.

**** **** ****
Mungu anamthibitishia Ibrahimu kwamba uzao wake utakuwa kama muvumbi yasiyohesabika.
Amembariki kuwa na uzao mkubwa sana. Ni agano la Mungu na Ibrahimu peke yake. Lakini cha kushangaza mkewe Ibrahimu akawa hapati mimba.
Ikawa changamoto kwake japo anaziishi baraka za Bwana maishani mwake.

Ibrahimu alifika hatua ya kuzaa na kijakazi wake baada ya kuona kama Sara hawezi tena kuzaa, ameshakuwa mzee.
Lakini hayo yalikuwa ni macho yake na sivyo kama aonavyo Mungu.

MWANZO 17:17
Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema moyoni, Je! Mtu wa umri wa miaka mia, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa?

**** **** ****
Wanadamu wanaweza kuona kama hujabarikiwa lakini umebarikiwa.

Unaweza ukajiona hujabarikiwa lakini umebarikiwa.

Changamoto na vitisho vya maneno ya watu visikutoe katika mpango wa Mungu.
Vyovyote utakavyokuwa unaendelea kumwamini Mungu hata kama unachekwa na watu.
Baraka zako zipo na umeshabarikiwa.
Endelea na hilo tumaini lako la milele.

MWANZO 18:12-14
Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee?

 BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee?

 Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani.

*** **** ****
Haijalishi unajionaje.
Haijalishi wanadamu wanakuonaje.
Bali inajalisha unaishi kwa misingi gani ndiyo ushindi wako.
Ikiwa tumaini lako ni kwa Mungu aliye juu basi hutapungukiwa kwake.
Wanadamu wanaweza kukuona umepungukiwa au dhaifu lakini kwa Mungu wewe ni hodari.

Njia zake hazichunguziki wala hawazi kile unachowazia wewe.
Ikiwa unamtumainia yeye amini umebarikiwa wala usitafute kutazamwa na wanadamu ikiwa yeye ameshakutazama na mkono wake umekushika.

MWANZO 21:1-3
BWANA akamjia Sara kama alivyonena, na BWANA akamfanyia kama alivyosema.

  Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu.

 Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia.

**** **** ****
Kwa mazingira ya kawaida watu waliosikia kwa Ibrahimu kwamba amebarikiwa na atakuwa taifa kubwa lazima waliugua kwa kicheko.
Walicheka sana kuona amezaa mtoto uzeeni tena mmoja.

MWANZO 22:15-18
Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

**** **** ****
Mungu anaapa na nafsi yake tena anamwapia mwanadamu na kumwambia atambariki.
Atambariki kwakuwa ametii maneno na sauti yake.
Amemfuata kumtumikia yeye.
Kama Mungu anaapa kuna nini tena?
Halafu angalia hapa anamwambia atambariki kwa kitu gani.
Atambariki katika uzao.
Kama nyota za mbinguni au mchanga ulioko pwani.
Yani atakuwa taifa kubwa.
Hapo Ibrahimu ameshabarikiwa kwa kuwa ameisikia sauti ya Mungu.

Cha kushangaza Sara alifariki na Ibrahimu akafariki bila kuziona hizo baraka. Wote Ibrahimu na Sara walifariki wakiwa na huyo mtoto mmoja tu wa ahadi ambaye ni Isaka.

Unafikiri wanadamu waliongea maneno mangapi?
Unadhani walikejeli kwa kiasi gani baraka alizosema amebarikiwa na Mungu?

Je Ibrahimu alikuwa amebarikiwa au hakubarikiwa?
Unahisi umebarikiwa au hujabarikiwa?

MWANZO 21:10-12
Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

**** **** ****
Kumbe unapobarikiwa wewe hata uzao wako utabarikiwa.
Humbe baraka huwa zinarithiwa.
Katika baraka zote Mungu alizomwahidi Ibrahimu hakuziona kabisa mpaka kufa kwake

 (Lakini alikuwa amebarikiwa)

Hapa Mungu anakuja kumwambia tena Ibrahimu kwamba Isaka amezirithi baraka zile.
Ule uzao alioahidiwa ataurithi Isaka.

TUANGALIE MUNGU ANASEMAJE KUHUSU ISAKA BAADA YA IBRAHIMU KUFARIKI.

MWANZO 25:11
Ikawa, baada ya kufa kwake Ibrahimu, Mungu akambariki Isaka mwanawe. Naye Isaka akakaa karibu ya Beer-lahai-roi.Uzao wa Ishmaeli.

**** **** ****
Hapa ndipo napojua kuwa akili za Mungu hazichunguziki kabisa.

Tuendelee kuangalia maajabu ya Mungu.

MWANZO 26:3-5
Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako.

 Nitazidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, nami nitawapa uzao wako nchi hizi zote, na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.

 Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu.

**** **** ****

Mungu anamwahidi tena Isaka ahadi ile ile aliyomwahidi Ibrahimu baba yake.

MWANZO 26:24
BWANA akamtokea usiku ule ule, akasema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu baba yako, usiogope, maana mimi ni pamoja nawe, nami nitakubarikia, na kuzidisha uzao wako kwaajili ya Ibrahimu mtumishi wangu.

**** **** ****

Kumtumikia kwako Mungu Leo kunaweza kuwa ni kama hazina na urithi kwa wanao.
Au uzee wako.
Maombi unayoomba Leo kwa kufunga yanaweza yakakusaidia baadae katika uzee wako wakati ambao huna tena uwezo wa kufunga kwaajili ya udhaifu wa mwili wako.
Unaweza ukaomba Mungu akubariki Leo ukawa unazishika hukumu zake lakini hizo baraka zikaja kuangukia kwa watoto wako.

MWANZO 25:21-27
Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.

 Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA.

 BWANA akamwambia,Mataifa mawili yako tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.

Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.

 Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau.

 Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.

 Watoto wakakua, Esau alikuwa mtu ajuaye kuwinda wanyama, mtu wa nyikani, na Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa hemani.

**** **** ****
Baada ya hawa watoto kuzaliwa Isaka alimbariki Yakobo.
Yakobo akashikilia urithi naye Isaka akafa kabla hajaliona hilo taifa kubwa lenye watu wasiyohesabika.

Akabaki Yakobo akitembelea kile kijiti cha zile baraka za Ibrahimu babu yake.

MWANZO 28:10-14
Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.

 Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.

 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.

 Na tazama, BWANA amesimama juu yake, akasema, Mimi ni BWANA, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako.

Na uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi, na mashariki, na kaskazini, na kusini; na katika wewe, na katika uzao wako, jamaa zote za dunia watabarikiwa.

**** **** ****
Yani mtu wa Mungu kama hujalisoma neno na kujifunza kwa bidii unaweza ukajihisi unalala na njaa kumbe umeshakula na umeshiba mno.
Unaweza ukamlalamikia Mungu kumbe ameshakupa mahitaji yako yote.
Usichoke kuomba wala usimpangie Mungu namna ya kuachia baraka zake katika maisha yako.
Mimi nimebarikiwa maana tumaini langu ni kwake yeye.
Omba Leo huenda wakafaidika watoto wako, wazazi wako, wajukuu hata vitukuu.

Lakini ikiwa ni kwa MAPENZI ya Mungu hata wewe unaweza kuyaishi maombi yako ya Leo.
Tulia na Mungu mwache atimize MAPENZI yake usimpangie.
Lakini pia yeye hubadili majira na nyakati.
Huzuru wafalme na nuru hukaa kwake.

Ahadi za Ibrahimu hakuzishuhudia na macho yake,
Ibrahimu akamuachia Isaka naye hakuzishuhudia kwa macho yake,
Isaka akamwachia Yakobo.

Hapa MUNGU anamtamkia Yakobo baraka zile zile alizomtamkia Ibrahimu.

Ni miaka mingi sana imeshapita lakini bado wanaishi kwenye kusudi la Mungu bila kujali kitatokea lini.

Tuone itakuwaje.

Halafu hizi roho za kufuatilia huwa zipo kabisa.

Tazama Ibrahimu alipata mtoto kwa shida sana yeye na Sara.

Isaka naye mke wake Rebeka alikuwa tasa na walipata uzao baada ya Isaka kumwomba BWANA juu ya mke wake.

Yakobo naye alikaa muda mrefu na Raheli bila kupata mtoto,
Baada ya kumwomba sana Mungu ndipo akamzaa Yusufu.

Raheli alijaribu pia kufanya kama Sara akamwambia Yakobo ampe uzao kwa mjakazi wake aliyeitwa Bilha.

Wote wawili Bilha na Lea aliyekuwa mdogo wake Raheli walizaa watoto wengi lakini utithi wa zile baraka za Mungu kwa Ibrahimu zilienda kwa Yusufu aliyekuwa mtoto wa Raheli.

Yakobo alikuwa na wanawake wawili ambapo mmoja ndiye aliyekuwa wa malengo yake aliyeitwa Raheli.
Huyo Lea alikuwa mke wake pia kwaajili ya Labani ambaye ni mjomba wake Yakobo kufanya hila na kumwozesha watoto wake wote wawili.

SOMA MWANZO SURA 28 MPAKA 30 YOTE.

MWANZO 35:9-12
Mungu akamtokea Yakobo tena, aliporudi kutoka Padan-aramu akambariki.

 Mungu akamwambia, Jina lako ni Yakobo; hutaitwa tena Yakobo, lakini Israeli litakuwa jina lako. Akamwita jina lake, Israeli.

 Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu , uzidi ukaongezeke. Taifa na kundi la mataifa watatoka kwako, na wafalme watatoka viunoni mwako.

 Na nchi hii niliyowapa Ibrahimu na Isaka nitakupa wewe, na uzao wako baada yako nitawapa nchi hiyo.

**** **** ****
Hakuna tofauti yoyote katika hizi ahadi za kubarikiwa.
Lakini hakuna aliyezishughudia hizi baraka kwa macho yake.
Kati ya Ibrahimu, Isaka, na Yakobo.

Lakini wanamtumikia na kumwabudu Mungu kwa uaminifu.

TUENDELEE

Yakobo alizaa watoto 12 ambaye haitwi tena Yakobo Mungu alishambadilisha jina na kumwita Israeli

 MWANZO 35:10

Kwahiyo sasa Yakobo tutamwita Israeli.

Ule urithi wa zile baraka za Ibrahimu ukaenda kwa  Yusufu mtoto wake Israel.

Kwahiyo Yusufu akawa ndiye anatembelea zile baraka na ahadi ya Mungu.

Yusufu yupo katika ahadi na baraka zote za Mungu lakini angalia kilichompata katika maisha yake.

Utahisi labda hajabarikiwa.

Ndugu zake walipogundua kuwa amebarikiwa na Mungu wakaamua kumwuza Misri kwa kuwa mtumwa ili ndoto yake isitimie.

MWANZO 37:5-8
Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;

 akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.

 Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.

 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake.

**** **** ****

Ndugu zake walijisikia vibaya juu ya ile ndoto yake wakapanga kumwuza kuwa mtumwa huko Misri.

MWANZO 37:26-28
Yuda akawaambia ndugu zake, Kwafaa nini kumwua ndugu yetu, na kuificha damu yake?

 Haya, na tumwuze kwa hawa Waishmaeli, wala mikono yetu isimdhuru, maana yeye ni ndugu yetu, na damu yetu. Ndugu zake wakakubali.

 Wakapita wafanya biashara Wamidiani; basi wakamtoa Yusufu, wakampandisha kumtoa katika birika, wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande vya fedha ishirini; nao wakamchukua Yusufu mpaka Misri.

**** **** ****

Ndugu zake walifanikiwa kumwuza na kuwa mtumwa kule Misri.

Lakini kwakuwa alikuwa na ahadi ya Mungu katika maisha yake alipata kibali machoni pa Farao.

Baadae njaa ikatokea dunia nzima ila Misri.

Njaa iliyowafanya ndugu wa Yusufu kwenda Misri kujitafutia chakula kwa kununua.

MWANZO 42:3-4
Basi ndugu kumi wa Yusufu wakashuka Misri ili wanunue nafaka.

 Walakini Benyamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumpeleka pamoja na ndugu zake, maana alisema, Mabaya yasimpate.

**** **** ****
Ndugu wa Yusufu walioshuka Misri walikuwa 10 akabaki Benyamini.
Kwahiyo ukijumlisha na Yusufu wanakuwa 12 ambao wote ni wana wa Yakobo(Israeli)

MWANZO 42:6-9
Naye Yusufu alikuwa ni liwali juu ya nchi, ndiye aliyewauzia watu wote wa nchi. Nao ndugu zake Yusufu wakaja, wakainama kifudifudi mbele yake.

 Yusufu akawaona nduguze, akawatambua, lakini alijifanya kama mgeni kwao. Akasema nao kwa maneno makali, akawaambia, Mmetoka wapi ninyi? Wakasema. Tumetoka nchi ya Kanaani, ili tununue chakula.

 Yusufu akawatambua nduguze, bali wao hawakumtambua yeye.

 Yusufu akazikumbuka zile ndoto alizowaotea. Akawaambia, Wapelelezi ninyi, mmekuja ili mwuone utupu wa nchi.

**** **** ****
Baada ya Yusufu kufungwa gerezani miaka mingi lakini baadae Mungu akampa kibali akamketisha na wakuu na hatimaye akawa liwali juuu ya Misri yote.
Tena alifungwa kwa kesi ya kusingiziwa.

Je, ni nani awezaye kupatwa na changamoto zote hizo halafu akajiona au watu wakamwona mbarikiwa?

Je, hawataanza kukukejeli wewe na Mungu unayemtumikia?

Ukijiona umesimama vizuri na Mungu usiangalie unachopitia wewe amini Mungu amekushika mkono.

TUENDELEE KUANGALIA ZILE BARAKA ZA IBRAHIMU ZIKO WAPI.

MWANZO 45:17-20
Farao akamwambia Yusufu, Uwaambie ndugu zako, Fanyeni hivi; wachukuzeni mizigo wanyama wenu, mwondoke mwende nchi ya Kanaani;

 kisha mkamtwae baba yenu, na watu wa nyumbani mwenu, mkanijie; nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.

 Nawe umeamriwa; fanyeni hivi, mjitwalie magari katika nchi ya Misri kwa watoto wenu wadogo na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.

 Wala msivisumbukie vyombo vyenu, maana mema ya nchi yote ya Misri ni yenu.

**** **** ****
MWANZO 46:1-4
Akasafiri Israeli, pamoja na yote aliyokuwa nayo, akaja Beer-sheba, akamchinjia sadaka Mungu wa Isaka babaye.

 Mungu akanena na Israeli katika ndoto ya usiku, akasema, Yakobo, Yakobo. Akasema, Mimi hapa.

 Akasema, Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako, usiogope kushuka mpaka Misri; maana nitakufanya uwe taifa kubwa huko.

 Mimi nitashuka pamoja nawe mpaka Misri; nami nitakupandisha tena bila shaka; na Yusufu ataweka mkono wake juu ya macho yako.

**** **** ****
Hapa sasa uzao mzima wa Ibrahimu wanashuka Misri na bado Mungu anamwahidi Israeli kwamba atamfanya kuwa taifa kubwa huko Misri.

MWANZO 47:5-6
Farao akamwambia Yusufu, akisema, Baba yako na ndugu zako wamekujia;

 nchi ya Misri iko mbele yako, palipo pema pa nchi uwakalishe baba yako na ndugu zako; na wakae katika nchi ya Gosheni. Tena ukijua ya kuwa wako watu hodari miongoni mwao, uwaweke wawe wakuu wa wanyama wangu.

**** **** ****
Israeli na wanawe wote 12 wakawa wanaishi Misri kwa kuikimbia njaa nchi ya Kanaani.
Na Mungu alishamwahidi kwenye ndoto kwamba atamfanya huko kuwa taifa kubwa.

MWANZO 48:21
Israeli akamwambia Yusufu, Angalia, mimi ninakufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, naye atawarudisha mpaka nchi ya baba zenu.

**** **** ****
Nchi ya baba yao Ibrahimu na Isaka ni nchi ya Kanaani na Israel anamwambia Yusufu kwamba Mungu atakuwa pamoja nao na watarudi.

Israeli akafa na Yusufu naye akafa, uzao wa wana wa Israeli ukaongezeka huko Misri

KUTOKA 1:6-9
Yusufu akafa, na ndugu zake wote, na watu wote wa kizazi kile.

 Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.Waisraeli Wateswa

 Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.

 Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi.

**** **** ****
Ule uzao uliongezeka isivyo kawaida mpaka wamisri wakawa na hofu kwamba watakuja kutawaliwa.

Wamisri wakawanyanyasa sana na kuwapa kazi ngumu.
Wakawa watumwa.

Walilia usiku na mchana kwa yale mateso waliyoyapata.
Pamoja na changamoto zote za kuteseka na kutumikishwa kazi ngumu lakini bado walikuwa na ahadi ya Mungu katika maisha yao.
Ni watu waliobarikiwa.
Pamoja na kubarikiwa kwao lakini walikuwa ni watu waliodharauliwa sana.

KUTOKA 1:15-17
Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua;

 akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi.

 Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume.

**** **** ****
Wamisri walitafuta kila njia za kuwapunguza ikashindikana.
Ahadi ya Mungu kwa Ibrahimu inaanza kuonekana.
Zile baraka za kuwa taifa kubwa ndiyo zinaanza kuonekana sasa.

(Mungu hubariki kwa mapenzi yake na njia zake hazichunguziki)

KUTOKA 2:5-10
Basi binti Farao akashuka, aoge mtoni, na vijakazi wake wakatembea kando ya mto; naye akakiona kile kisafina katika majani, akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta.

 Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.

Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu?

Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto.

Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha.

Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini.

**** **** ****
Katika Mungu kuitimiza ahadi yake kwa Ibrahimu akamwinua Musa naye akamtuma kwenda kuwatoa wana wa israeli kutoka huko utumwani Misri walikokuwa wanateseka.

Wakavuka bahari kwa ishara na ajabu nyingi.

Mpaka Leo hii sisi tulio wakristo ndiyo uzao wa Ibrahimu.

Je, sisi ni taifa kubwa au siyo?

Baraka alizoahidiwa Ibrahimu ndizo zilikuja kutimia kwa (YAKOBO)Israeli.

Ndiye huyo Mungu tunayemwabudu sisi Mungu wa Israeli.

Unaweza ukahisi hujabarikiwa kulingana na maisha unayoishi.

Ibrahimu aliamini kubarikiwa na kuwa taifa kubwa japo alikuwa na mtoto mmoja tu wa ahadi na akafa bila kuona chochote.

Ikiwa wewe unamwabudu Mungu kwa kweli na uaminifu amini hauko peke yako.

Ilimradi uwe mwaminifu mbele zake.
Kama ungefunuliwa macho yako Mungu akuonyeshe baraka zilizopo mbele yako ungemtukuza Mungu mchana na usiku.
Hata kama umekuwa mwaminifu kwa Mungu kwa muda mrefu na hujaona chochote mpaka uzeeni, wewe amini baraka zako zipo na usimpangie Mungu namna au majira ya kuzidhihirisha au kuzithibitisha hizo baraka.

ENDELEA KUMWABUDU MUNGU MAANA WEWE NI MBARIKIWA KWA JINA LA YESU KRISTO.

MUNGU HAMTUPI MTU.
BALI HUBARIKI KWA MAPENZI YAKE NA WAKATI WAKE.
NA PIA ANASEMA NJIA ZAKE SI KAMA ZETU NA AKILI ZAKE HAZICHUNGUZIKI.

#Powered_by_Holly_Spirt

NGUVU YA KUISHINDA DHAMBI NA MATENDO YOTE MABAYA.

BWANA YESU ASIFIWE NA KUPEWA UTUKUFU WOTE.

Kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Leo tunajifunza somo lenye kichwa kinachosema,

NGUVU YA KUISHINDA DHAMBI NA MATENDO YOTE MABAYA.

Kwa sisi wateule wa Mungu tulionunuliwa kwa damu ya Yesu Kristo tena damu ya thamani huwa tunaugua sana tunapojikuta tumeanguka katika dhambi.
Lakini leo Roho Mtakatifu yuko hapa na sisi kwa ajili ya kutusaidia katika madhaifu yetu.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

Neno la msingi katika mafundisho yetu.

METHALI 4:23
Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

*************
Moyo ndiyo kitu cha kulinda sana kuliko vitu vyote maana uzima uko ndani yake.
Moyo unapoharibika basi utakuwa huna tena uzima ndani yako.
Chemchemi za uzima ni ule uwezo wa kutenda mema tu.
Maana katika msamaha wa dhambi kuna nguvu ya uponyaji ndani yake.
Yesu anasema kuwa alikuja ili tuwe na uzima tena tuwe nao tele.
Lakini kubwa zaidi alikuja ili kumkomboa mwanadamu katika dhambi.
Yesu anapokuwa moyoni mwako hiyo ndiyo chemchemi ya uzima ndani yako.
Unaposamehewa tu dhambi na moyo wako kuwa safi basi hata magonjwa yanakimbia.

ISAYA 33:24
Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.

****************
Hivyo Chemchemi za uzima zitakapokuwa moyoni mwako ambozo ni Yesu Kristo aliye msamaha wa dhambi basi kuugua kutakimbia kabisa, Yesu ndiye njia na kweli na UZIMA.
Uzima wa MTU upo ndani ya Yesu na ndiyo maana anasema pia aniaminiye mimi hata atakapokufa ataishi.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

ZABURI 119:11
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako,Nisije nikakutenda dhambi.

****************
Huyu mwandishi wa Zaburi anasema ameliweka neno la Mungu moyoni ili asitende dhambi akiwa na maana kwamba ukishamweka Yesu (Neno) moyoni mwako hutatenda dhambi tena maana neno likijaa moyoni mwako kila utakachofanya biblia inakuwa ni muongozo mzuri sana kwako na utakapotii hutatenda dhambi.

Ukiwa na Yesu ndani yako atakupa Yule msaidizi ambaye ni Roho wa kweli aliyetuahidi na atatusaidia katika mambo yote.
Yesu ndiye aliyetuahidi sisi walio wake kwamba hatatuacha yatima bali atamwomba baba atupe msaidizi.
Sasa kama hujaokoka ili uwe wa Yesu naye akupe msaidizi wa kuishinda dhambi wala usijidanganye kwamba hutendi dhambi.

YEREMIA 17:9
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

*****************
Iko hivi
Kama hujaokoka basi hujampata Yesu katika maisha yako.
Na kama hujampata Yesu huna nguvu yoyote ya kushinda dhambi maana moyoni mwako neno halipo.
Na Yesu ndiye anayekupa Roho wa kukuongoza katika mambo yote.
Usijidanganye kwamba hutendi dhambi maana moyo ni mdanganyifu na kamwe wewe huwezi kuujuwa.
Wewe huna uwezo wowote wa kuujuwa moyo wako.
Yesu peke yake ndiye anayejuwa kama moyo wako ni mkamilifu au unakudanganya.
Yesu akiwa moyoni mwako ndipo utajijuwa kama una dhambi au huna.
Moyo unaweza kukuaminisha kitu cha ajabu sana wala usibadilishwe na mtu yeyote hivyo ili moyo wako uwe na kibali mbele za Mungu ni lazima ndani yake ulijaze neno lake, Yesu akae moyoni mwako kila wakati.

METHALI 18:12
Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

***************
Mtaji wa kwanza kwa mtu anayetaka kufanikiwa ni WAZO.
Lile wazo linatoka ndani ya moyo.
Sasa moyoni mwako Yesu yupo ili litoke wazo jema?
Kama shetani ndiye aliye moyoni mwako basi litatoka wazo baya tu.

Unapoona unatumia simu yako unaona ni jambo la kawaida ujue kuna mtu alianzisha wazo kutoka moyoni akalitendea Kazi.

Unapoona nchi yenye vita watu wanauwana ujue kuna mtu mmoja alitoa wazo moyoni mwake ambako hakukuwa na chemchemi za uzima ndiyo maana maovu yanatendeka.

Ukiona upo huru hutawaliwi ujue kuna mtu alitoa wazo moyoni mwake akaanza kupigania Uhuru watu wakakombolewa.

Unapomuona Yesu Kristo anatenda mambo kwetu makubwa na ya ajabu watu wanaokoka na kukombolewa katika maovu ujue ni Mungu aliwaza akaona amtoe mwanae wa pekee ili kila amwaminiye aokolewe katika yeye.

Ukiona mtu anateseka, anajuta, ameanguka, Hana amani, vita, na mambo mengine ya uharibifu basi ujue kabla ya mtu huyo kuwa hivyo moyo wake ulijivuna.
Shetani yuko hivi leo kwasababu alijiinua na kuwa na kiburi na majivuno moyoni mwake.

Ukiona mtu anaheshimika, amefanikiwa, ameokoka na kumpokea Yesu, amekuwa na utajiri udumuo na wenye amani, basi ujue moyo wake ulikuwa mnyenyekevu.

MATHAYO 11:29
Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

*****************
Yesu anasema tujifunze kwake, ni mpole na mnyenyekevu wa Moyo.
Raha tuliyo nayo na mamlaka tulizo nazo ni kutokana na unyenyekevu wa moyo wake.
Alitii yote hata mauti ya msalaba.
Hakuna mahali popote ambapo Yesu alikuwa mkaidi mpaka alipofika msalabani.
Ule unyenyekevu wa Moyo wake ndiyo uliomsaidia kushinda na dunia ikaokolewa.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

1WAFALME 11:1-3
Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti,

na wa mataifa BWANA aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda.

Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.

*****************
Pamoja na Sulemani kumpenda Mungu lakini uharibifu ulipoingia moyoni mwake alibadilika mpaka kuabudu miungu.
Hakuulinda moyo wake.
Unapokuwa na mahusiano na mwanamke huwa mnakuwa mwili mmoja hivyo unakuwa na tabia za kwake na utajikuta unafanana naye.
Linda moyo wako kuliko yote ulindayo.
Dhambi zote zinaanzia moyoni.

LUKA 6:45
Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

*****************
Ukitaka kumjuwa mtu ana tabia gani moyoni mwake au anawaza nini basi msikilize maneno yake.
Moyo husema kupitia kinywa maana ulimi hufichua siri za moyoni.
Ukiwa na kitu moyoni halafu ukakaa na mtu mkaongea kwa dakika chache atajuwa kilichopo moyoni mwako.
Kama una kisasi na mimi ukikaa na mimi tukiongea lazima nitakujuwa tu.
Kama unanipenda nikikaa nikiongea na wewe nitakujuwa tu.
Kama nikisikiliza wingi wa maneno yako ukawa unaongelea jambo fulani tu basi dhahiri hayo ndiyo maisha yako.

MATHAYO 9:20-22
Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.

******************

Tazama wazo la moyoni la huyu mwanamke namna lilivyobadili kabisa historia ya maisha yake.
Mawazo ya moyo wa huyu mwanamke yalikuwa ni uponyaji kupitia Yesu Kristo na alimweka moyoni akamwamini na kweli akapata uponyaji na Yesu akawa ndani yake.

Sasa wewe umemweka nani moyoni mwako juu ya changamoto ulizo nazo?
JIPANGE.
Kilichopo moyoni mwako ndicho kitakachokukomboa.

MATHAYO 6:21
kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.

******************
Kwa sasa unamtumikia nani?
Unamwamini nani katika maisha yako?
Umeweka hazina yako kwa waganga?
Umejiwekea hazina yako kwa wanadamu?
Kila unachofanya utalipwa haijalishi ni kibaya au kizuri.
Kama ukifanya mema Mungu Baba kwa jina la Yesu Kristo atakulipa mema.
Lakini ukifanya uovu utalipwa na huyo huyo mwovu.
Weka hazina yako kwa Yesu Kristo nawe utaikuta Mbinguni mpendwa.
Maisha haya ni mafupi sana hayakawii kwisha.
Ulikojiwekea hazina yako ndiko moyo wako uliko.
LINDA SANA MOYO WAKO.

KUSHINDA DHAMBI

ZABURI 19:14
Maneno ya kinywa changu,Na mawazo ya moyo wangu,Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA,Mwamba wangu, na mwokozi wangu.

****************
Tumeshaona chanzo cha jambo lolote kuwa ni mawazo ya moyo.
Hata shetani anapotaka kukuingia huwa anakupa wazo halafu unapoanza kulitafakari anakupa majibu na kisha unatenda.

Mfano mzuri ni mawazo ya kuzini huwa ni mabaya sana.
Unaweza ukawa umekaa unaanza kuwaza ngono tu moyoni mwako.
Sasa ukiendelea kuwaza kwa muda Fulani na mwili unapokea lile ombi kisha unajikuta umeshazama kabisa na kutoka hutaweza tena.

WAEFESO 4:27
wala msimpe Ibilisi nafasi.

***************
Unapojipa nafasi ya kuwaza uovu kwa muda mchache huwa shetani anakupa mbinu za ushindi na utajikuta tu umechukua maamuzi.

Ukijiona tu kuna wazo linaingia moyoni mwako ambalo halina kibali mbele za Mungu au halimpendezi Mungu basi usijipe kabisa hata sekunde kumi za kuendelea kulichanganyua.
Kama ukiendelea kulitafakari utafanya maamuzi yasiyo na kibali mbele za Mungu na utakuja kujuta baadae.
Kabla hujaongea chochote kwanza jiulize Mungu atafurahia nachokisema?
Mwandishi ameanza kumwomba Mungu kuhusu maneno ya kinywa chake maana ukishaanza kuongea uovu ndipo na moyo utatafakari huo uovu na shetani huja kuutia nguvu ili ufanye maamuzi yasiyo mpendeza Mungu.
Kama huamini anza sasa kuwaza jambo fulani kwa muda wa dakika kumi bila kuingiza mawazo mengine yoyote uone utachukua maamuzi gani.
Halafu kama kuna tabia Fulani imekushinda kabisa kuiacha anza leo, ukiona wazo la kufanya ile tabia linakujia usilifikirie tena uone kama utaifanya tena.

Hata watu wa matangazo huwa wanatumia mbinu hii.
Wanarusha tangazo lao kwenye vyombo vyote vya habari.
Halafu linakuwa linarushwa kila wakati na watu wanashawishika na kujikuta hata wamekaririshwa kwa lazima na ukishaanza kuliwazia kwa undani utanunua ile bidhaa au utaona ni bora japo hutaki au huna fedha za kununulia.
Kama usingeendelea kusikiliza yale matangazo wala usingeipenda ile bidhaa.

Kuna wimbo ulipousikia kwa mara ya kwanza uliuona sio mzuri masikioni mwako lakini baada ya kuusikia mara kwa mara mpaka umejikuta sasa hivi umeufanya mwito wa simu yako.
Kama usingekuwa unaendelea kuusikia bila Shaka usingeupenda.

Jizuie kuwaza uovu pindi tu wazo la huo uovu linapokujia na utafanikiwa kuishinda dhambi.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

#Powered_By_Holly_Spirit

Tuesday 1 May 2018

SIMAMA KATIKA NAFASI YAKO KUMTUMIKIA MUNGU.

BWANA YESU ASIFIWE

Kwaajili ya sifa na utukufu wa Mungu Baba kwa jina la Yesu Kristo nakuletea somo lenye kichwa kinachosema,

SIMAMA KATIKA NAFASI YAKO KUMTUMIKIA MUNGU.

Dunia imesimama katika nafasi yake huku yule mwovu naye akisimama imara kuhakikisha kwamba anawapata walio wake.
Lakini inatubidi na sisi tuliofanyika kuwa wana wa Mungu tusimame imara kuhakikisha kwamba tunamshinda kwa kuwafungulia dhambi wale waliofungwa.
Ni wazi kwamba unaposimama katikati ya mataifa na kuongea kweli kuhusu huyu Yesu utapingwa na kudhihakiwa na wengi lakini tusife moyo wana wa Mungu.

TWENDE KWENYE NENO LA MSINGI WA MAFUNDISHO YETU.

MATHAYO 5:11-12
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

****************

Wakati unapomtamka Mungu huwa shetani haimpi shida yoyote na hata watu watakusikiliza kwa makini sana kana kwamba wanataka kujifunza.
Hata shetani anajijuwa kabisa hawezi kupambana na Mungu, anajijuwa pia hana uwezo wa kupambana na Yesu.
Anachojitahidi yeye ni kuhakikisha anaweka uvuli kwa hao unaowahubiria ili tu wasije wakaikubali hiyo damu ya Yesu ambayo iko katika wokovu.
Hataki kwenda jehanamu peke yake.

Utasemwa vibaya kwaajili ya jina la Yesu na hata tunaona namna ambavyo hata baadhi ya huduma zetu zinavyopigwa vita na anadhiriki kutengeneza hata manabii wake wa uongo na wanapofanya jambo lililo kinyume analifanya lijulikane na kila mtu ili hilo jambo liwe sababu ya watu kutokuziamini huduma nyingine za Yesu Kristo.
Jiulize ni kwanini mtumishi wa kweli anapofanya jambo jema asiongelewe na kujulikana na kila mtu?

Lakini hata kama ukisemwa vibaya na watu kuanza kukufikiria kwa namna yao wewe endelea kuhubiri tena kwa bidii zaidi maana ndicho kilichomfanya Mungu akuite kwa jina lake.

1WAKORINTHO 15:58
Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.

***************

Tuendelee kuchapa injili ya Yesu na kumfikishia habari kila mmoja ili baadae asije akajitetea kwamba hakusikia.
Utachekwa mara nyingi sana kuonekana masikini uliyekosa Kazi lakini nakuambia hutachekwa bure.
Yani wanadamu wamekuwa wa ajabu sana.

Unaweza ukawa umesimama mahali unahubiri halafu pembeni yako akawa amesimama kahaba aliyevaa nguo za aibu yuko uchi mwili mzima lakini utashangaa kati yenu wawili watu wanakuona wewe ndiye kituko.
Mungu atusaidie sana tuendelee maana hii kazi siyo bure.
Ipo siku ile moja tu ya kupepeta makapi na ngano na hapo wako watakaolaani hata matumbo ya mama zao na wote watatamani kama wangehubiri.
Sisi tunaoijuwa kweli hatutaki mtu ajute siku hiyo na ndiyo maana huwa tunahangaika kuhakikisha watu wanampokea Yesu na kuachana na dhambi.

2WAKORINTHO 4:3-4
Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;

Ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.

********************

Huyu shetani anaakili nyingi sana mpaka Mungu anamtunuku jina
 (mungu wa dunia hii)
Fikra za watu zimepofushwa hawataki kabisa kuipokea injili ya kweli.
Mtu akilazimika saana basi atamkiri Yesu lakini atakuambia lakini mimi siiachi dini yangu.
Shetani ni mbaya mno.
Anakuambia tu Mungu haangalii dini au unakoabudu bali anaangalia moyo.
Analiongea andiko kuubwa kwa namna ya kawaida kabisa na anajiona yuko sahihi.
Mpendwa usije ukafikiri kuna mtu aliyeokoka na bado yuko kwenye dini na wala usidhani hizi dini zilizopo unazodhani zinamwabudu Mungu kwamba ipo hata moja Mungu anayopendezwa nayo.
Ni mungu wa dunia hii anapofusha fikra zako.
Angalia hata hilo jina mungu limeandikwa kwa kuanza na herufi ndogo likimaanisha kwamba anayetajwa hapo ni shetani ibilisi.

Unavyokataa injili ya Yesu usidhani hata kama angekuja nabii wa zamani ungemwelewa.
Tatizo lililopo kwako siyo Yule anaekuhubiria bali ni huyo anayekuzuia wewe kuelewa ili usije ukoelewa ukaokoka akakukosa.

YEREMIA 1:5-10
 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.

Lakini BWANA akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.

Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema BWANA.

Ndipo BWANA akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; BWANA akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;

Angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung?oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.

******************
Huyu nabii Yeremia alipata wakati mgumu sana katika kipindi chake.
Lakini ukisoma maandiko ukimfuatilia jinsi Mungu alivyomwahidi huthanii kama ndiye huyo anaepitia changamoto kubwa namna hii.
Nikimsoma huwa napata nguvu ya kumhubiria mtu yeyote.
Mungu alimthibitishia kabisa mwamba ametia maneno yake kinywani mwa Yeremia.
(yaani akiongea ni Mungu kaongea)
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

YEREMIA 20:7-9
Ee BWANA, umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki.

Maana kila ninenapo napiga kelele, nalia, Dhuluma na uharibifu! Kwa kuwa neno la BWANA limefanywa shutumu kwangu, na dhihaka, mchana kutwa.

Nami nikisema, Sitamtaja, wala sitasema tena kwa jina lake; basi, ndipo moyoni mwangu kumekuwamo kama moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia.

*****************
Cha kushangaza kila Yeremia alipopewa unabii kwaajili ya taifa la Israeli watu walimdhihaki na kumwona kituko.
Mpaka Yeremia anadhiriki kumwambia Mungu kwamba amemhadaa.
Lakini siyo kweli kwamba Mungu alimhadaa.
Watu wanamshutumu wanamwona si kitu mbele yao.
Alitamani sana aache kuongelea habari za Mungu kabisa lakini haikuwa rahisi.

Watu wanafikiri labda sisi tunatumia muda wetu mwingi kuwahubiria ili tupate kitu kutoka kwao.
Hayo ni mawazo kamili ya shetani.
Wewe unaehubiriwa siku ukiijua kweli halafu ukamhubiria mtu akakataa utatamani hata umpige lakini sisi huwa tunampiga na upanga ambao ni neno la Mungu.
Vita vyetu si ju ya damu na nyama bali ni katika falme na mamlaka.
Utatamani kumpiga maana anavyoikataa kweli uliyofundishwa na Yesu unamwona kama mfu lakini yeye anakuona wewe ndiye kichaa.

Yeremia anasema sitamtaja tena Mungu maana natukanwa na kufanyiwa kila aina ya dhihaka.
Lakini anaposema hatamtaja ndivyo anavyozidi kuumia zaidi anapoona watu wanapotea huku yeye akiijuwa njia.
Ndugu zangu sisi tunaoijuwa kweli tunapokueleza ukapuuza huwa tunaugua haswa.
Tuoneeni huruma muokoke mtatuuwa.

Huwa kweli tunahisi kama moto unawaka ndani yetu.

WAEBRANIA 12:29
Maana Mungu wetu ni moto ulao.

***************

Lile neno la kweli linapokaa ndani yetu halafu tukaamua kunyamaza kwaajili ya kejeli na matusi yenu huwa linatulazimu kutoka kivyovyote maana Mungu huwa haliweki ndani yetu ili likae bila kuponya watu.

Mimi sitaacha kufundisha injili ya kweli hata iweje na wala siwezi kunyamaza.
Nitasimama katika nafasi yangu na panapohitajika neema ya Yesu basi itashuka.

Usiache kabisa kuifanya Kazi ya Mungu kwaajili ya wanadamu.
Mungu anapokutuma kwenda kuifanya huwa anajuwa kila kitu mwisho wake kabla hata wewe hujaujua mwanzo.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

EZEKIELI 2:5-6
Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao.

Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.

*****************
Mungu anawajuwa kabisa.
Wako watakaoielewa hiyo injili lakini wanaamua kuwa na mioyo migumu kwa makusudi kwakuwa wana mambo yao na wanadhani hawawezi kuyaacha na hayachangamani na wokovu.

Mungu anajuwa kabisa huko alikokutuma na kwa watu walioasi na anakuambia kuwa usifadhaike kwaajili ya hayo utakayotendewa ikiwa wamekukataa wewe kung'uta mavumbi ya miguu yako uyaacha pale.
Daima endelea kusimama katika nafasi yako sawasawa hata katika marafiki zako na ndugu na jamaa asije akawepo hata mmoja akaja kukulaumu kwamba hukumwambia.

EZEKIELI 33:7-9
Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu.

Nimwambiapo mtu mbaya, Ewe mtu mbaya, hakika utakufa, nawe husemi neno la kumwonya mtu huyo, aiache njia yake, mtu mbaya huyo atakufa katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

Walakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako.

****************

Mpendwa kama neno la Mungu likijaa ndani yako sawasawa hutapata nafasi ya kulala bali utakuwa unalia kila wakati kwa wale wanaolikataa.
Lutu aliwaambia wakwe zake twendeni tuondoke maana huu mji utaangamizwa, lakini alikuwa kama kichekesho kwao wakadharau na baadae waliangamia katika ule moto.
Vivyo hivyo Nuhu alipokuwa akijenga safina alionekana kichekesho lakini baadae walewale waliokuwa wakimcheka waliangamia.

Usipowaambia watu ukweli kuhusu Yesu ujue utahukumiwa wewe.
Bali ukiwaambia wakikataa watajihukumu wenyewe.

NEHEMIA 5:19
Unikumbukie, Ee Mungu wangu, kwa mema, yote niliyowafanyia watu hawa.

******************

Wala usijali utakapowaambia wakakataa, wewe waambie huku ukiendelea kumwomba Mungu atakukumbuka kwa wakati wake.
Mwisho wa ubaya ni aibu pia karama ya dhambi ni mauti lakini pia wema hauozi wewe dimana katika nafasi yako.

UFUNUO 22:11-12
Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

*****************

Zidi kuitenda haki ya Mungu na mwenye kuacha matendo mabaya na ayaache na anayechagua matendo mabaya na aendelee lakini muda wa kujuta upo kabisa.
Ujira wako upo endelea kumwamini Mungu naye atakulipa kama Kazi yako ilivyo.
Chapa injili tena ikiwezekana pita nyumba hadi nyumba na ukifukuzwa ndipo unazidi kuinuliwa.
Cha msingi tu wewe unapoenda kwa mtu omba kibali kwa Mungu ili akupe msaidizi usiende peke yako.
Kazi yako wewe ni kuhubiri injili ya kweli lakini kuokoa muachie Yesu.

YOHANA 14:16-18
Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.

Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.

**************
Unapoenda kuhubiri ukiwa na huyo Roho ambaye ni msaidizi atalithibitisha neno mioyoni mwao na wakiamua kuokoka wataokoka lakini wakiamua kugeuza mioyo yao kuwa migumu basi mshukuru Mungu na uwe unawaombea.
Usipofanya hivyo utajikuta hata wokovu ulionao unakosa nguvu hata baadae kuanguka kabisa.

YOHANA 15:1-5
Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.

Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.

Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.

Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

***************

Yesu anajifananisha na mti wa mzabibu halafu baba yake ni mkulima.
Unapokuwa umeokoka unakuwa ni tawi katika ule mti wa mzabibu.
Na ni kweli kwamba mkulima yeyote anapotaka mti uzae vizuri huwa anatoa yale matawi dhaifu ili yasiyanyime yale matawi imara nafasi ya kuzaa vyema.
Ukikaa ndani ye Yesu sawasawa naye atakaa ndani yako na atakupa Roho msaidizi na ukimhubiria mtu ni lazima ataokoka.
Anaweza asiokoke siku hiyo lakini Yesu ambae ni neno likikaa ndani yako litakuelekeza kumwombea na ipo siku lile neno ulilomwambia litakuja kuhuishwa na Roho mtakatifu ndani yake na ataokoka.
BWANA YESU ASIFIWE SANA.

Huwezi ukasema umeokoka huku unamficha huyo Yesu wako wala humshuhudii kwa watu.
Kama huna jitihada za kuwafanya wengine waokoke ujue wokovu wako uko mashakani na wewe utakatwa maana ni tawi lisilozaa.
Yesu hajakuokoa tu bali amekuokoa ili akutumie katika ufalme wake.

Watu ambao shetani anawatumia wanafanya Kazi kwa bidii usiku hawalali na hawapati chochote sasa inashangaza sana wewe unaetumika na Mungu tena umeokolewa unasemaje umeokoka halafu upoupo tu?
Hakuna wokovu wa namna hiyo inabidi ubadilike na ujitathimini na wokovu wako uko wapi.

ASANTE SANA MUNGU BABA WA BWANA WETU YESU KRISTO NA ROHO WAKO MTAKATIFU ULIYE MFANYA KUWA MSAIDIZI NDANI YANGU KATIKA SOMO HILI.
NAOMBA PIA HILI SOMO LIKAHUISHWE KATIKA MIOYO YA WATU WAKO KWA JINA LA YESU KRISTO.
Ameeeen

#Powered_By_Holly_Spirit